10 Basi, wale wasichana wapumbavu walipokwenda kununua mafuta, bwana arusi akafika, na wale wasichana waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye katika jumba la harusi, kisha mlango ukafungwa.
11 Baadaye wale wasichana wengine wakaja, wakaita: ‘Bwana, Bwana, tufungulie!’
12 Lakini yeye akawajibu, ‘Nawaambieni kweli, siwajui nyinyi.’”
13 Kisha Yesu akasema, “Kesheni basi, kwa maana hamjui siku wala saa.
14 “Wakati huo itakuwa kama mtu mmoja aliyetaka kusafiri ngambo: Aliwaita watumishi wake, akawakabidhi mali yake.
15 Alimpa kila mmoja kadiri ya uwezo wake: Mmoja fedha talanta tano, mwingine talanta mbili na mwingine talanta moja, kisha akasafiri.
16 Mara yule aliyekabidhiwa fedha talanta tano akafanya kazi nazo akapata faida talanta tano.