12 niliyemtuma kwako, yeye mwenyewe, maana ni moyo wangu hasa;
13 ambaye mimi nalitaka akae kwangu, apate kunitumikia badala yako katika vifungo vya Injili.
14 Lakini sikutaka kutenda neno lo lote isipokuwa kwa shauri lako, ili kwamba wema wako usiwe kama kwa lazima, bali kwa hiari.
15 Maana, labda ndiyo sababu alitengwa nawe kwa muda, ili uwe naye tena milele;
16 tokea sasa, si kama mtumwa, bali zaidi ya mtumwa, ndugu mpendwa; kwangu mimi sana, na kwako wewe zaidi sana, katika mwili na katika Bwana.
17 Basi kama ukiniona mimi kuwa mshirika nawe, mpokee huyu kama mimi mwenyewe.
18 Na kama amekudhulumu, au unamwia kitu, ukiandike hicho juu yangu.