19 Lakini sikumwona mtume mwingine, ila Yakobo, ndugu yake Bwana.
20 Na hayo ninayowaandikia, angalieni, mbele za Mungu, sisemi uongo.
21 Baadaye nalikwenda pande za Shamu na Kilikia.
22 Lakini sikujulikana uso wangu na makanisa ya Uyahudi yaliyokuwa katika Kristo;
23 ila wamesikia tu ya kwamba huyo aliyetuudhi hapo kwanza, sasa anaihubiri imani ile aliyoiharibu zamani.
24 Wakamtukuza Mungu kwa ajili yangu.