20 Na hayo ninayowaandikia, angalieni, mbele za Mungu, sisemi uongo.
21 Baadaye nalikwenda pande za Shamu na Kilikia.
22 Lakini sikujulikana uso wangu na makanisa ya Uyahudi yaliyokuwa katika Kristo;
23 ila wamesikia tu ya kwamba huyo aliyetuudhi hapo kwanza, sasa anaihubiri imani ile aliyoiharibu zamani.
24 Wakamtukuza Mungu kwa ajili yangu.