28 wakisema, Mwalimu, Musa alituandikia ya kuwa, mtu akifiwa na ndugu yake mwenye mke, lakini hana mtoto na amtwae huyu mke, ampatie ndugu yake mzao.
29 Basi, kulikuwa na ndugu saba. Wa kwanza alioa mke, akafa hana mtoto;
30 na wa pili [akamtwaa yule mke, akafa hana mtoto;]
31 hata wa tatu akamwoa, na kadhalika wote saba, wakafa, wasiache watoto.
32 Mwisho akafa yule mke naye.
33 Basi, katika ufufuo atakuwa mke wa yupi? Maana aliolewa na wote saba.
34 Yesu akawaambia, Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa;