24 Yakatokea mashindano kati yao, kwamba ni nani anayehesabiwa kuwa mkubwa.
25 Akawaambia, Wafalme wa Mataifa huwatawala, na wenye mamlaka juu yao huitwa Wenye fadhili;
26 lakini kwenu ninyi sivyo; bali aliye mkubwa kwenu na awe kama aliye mdogo; na mwenye kuongoza kama yule atumikaye.
27 Maana aliye mkubwa ni yupi? Yeye aketiye chakulani, au yule atumikaye? Siye yule aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye.
28 Nanyi ndinyi mliodumu pamoja nami katika majaribu yangu.
29 Nami nawawekea ninyi ufalme, kama vile Baba yangu alivyoniwekea mimi;
30 mpate kula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu; na kuketi katika viti vya enzi, huku mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.