4 Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao.
5 Wakafurahi, wakapatana naye kumpa fedha.
6 Akakubali, akatafuta nafasi ya kumsaliti kwao pasipokuwapo mkutano.
7 Ikafika siku ya mikate isiyotiwa chachu, ambayo ilipasa kuchinja pasaka.
8 Akawatuma Petro na Yohana, akisema, Nendeni, mkatuandalie pasaka tupate kuila.
9 Wakamwambia, Wataka tuandae wapi?
10 Akawaambia, Tazama, mtakapoingia mjini mtakutana na mwanamume akichukua mtungi wa maji; mfuateni mkaingie katika nyumba atakayoingia yeye.