62 Akatoka nje akalia kwa majonzi.
63 Na wale watu waliokuwa wakimshika Yesu walimfanyia dhihaka, wakampiga.
64 Wakamfunika macho, kisha wakamwuliza-uliza wakisema, Tabiri, ni nani aliyekupiga?
65 Wakamtolea na maneno mengine mengi ya kumtukana.
66 Hata kulipokucha, walikutanika jamii ya wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, wakamleta katika baraza yao, wakisema,
67 Kama wewe ndiwe Kristo, tuambie. Akawaambia, Nijapowaambia, hamtasadiki kabisa.
68 Tena, nikiwauliza, hamtajibu.