17 Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]
18 Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.
19 Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina iliyotokea mjini, na kwa uuaji
20 Basi Pilato alisema nao mara ya pili, kwa vile alivyotaka kumfungua Yesu.
21 Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulibishe. Msulibishe.
22 Akawaambia mara ya tatu, Kwa sababu gani? Huyu ametenda uovu gani? Sikuona kwake hata neno lipasalo kufa. Basi nikiisha kumrudi nitamfungua.
23 Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana, wakitaka asulibiwe. Sauti zao zikashinda.