48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.
49 Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.
50 Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki.
51 Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni.
52 Wakamwabudu; kisha wakarudi Yerusalemu wenye furaha kuu.
53 Nao walikuwa daima ndani ya hekalu, wakimsifu Mungu.