27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu.
28 Na ijapokuwa hawakuona sababu ya kumfisha wakamwomba Pilato auawe.
29 Hata walipokwisha kumaliza yote aliyoandikiwa, wakamtelemsha katika ule mti, wakamweka kaburini.
30 Lakini Mungu akamfufua katika wafu;
31 akaonekana siku nyingi na wale waliopanda naye kutoka Galilaya hata Yerusalemu, ambao sasa ndio walio mashahidi wake mbele ya watu.
32 Na sisi tunawahubiri habari njema ya ahadi ile waliyopewa mababa,
33 ya kwamba Mungu amewatimizia watoto wetu ahadi hiyo, kwa kumfufua Yesu; kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili,Wewe ndiwe Mwanangu, mimi leo nimekuzaa.