45 Nami, kwa sababu nasema iliyo kweli, hamnisadiki.
46 Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki?
47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.
48 Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo?
49 Yesu akajibu, Mimi sina pepo; lakini mimi namheshimu Baba yangu, na ninyi mwanivunjia heshima yangu.
50 Wala mimi siutafuti utukufu wangu; yuko mwenye kutafuta na kuhukumu.
51 Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele.