27 na Abramu, naye ndiye Ibrahimu.
28 Wana wa Ibrahimu; Isaka, na Ishmaeli.
29 Hivi ndivyo vizazi vyao; mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, Nebayothi; kisha Kedari, na Abdeeli, na Mibsamu;
30 na Mishma, na Duma, na Masa, na Hadadi, na Tema;
31 na Yeturi, na, Nafishi, na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.
32 Na wana wa Ketura, suria yake Ibrahimu; yeye akamzaa Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani, na Ishbaki, na Shua. Na wana wa Yokshani; Sheba na Dedani.
33 Na wana wa Midiani; Efa, na Eferi, na Hanoki, na Abida, na Eldaa. Hao wote ndio wana wa Ketura.