31 na Yeturi, na, Nafishi, na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.
32 Na wana wa Ketura, suria yake Ibrahimu; yeye akamzaa Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani, na Ishbaki, na Shua. Na wana wa Yokshani; Sheba na Dedani.
33 Na wana wa Midiani; Efa, na Eferi, na Hanoki, na Abida, na Eldaa. Hao wote ndio wana wa Ketura.
34 Na Ibrahimu naye akamzaa Isaka. Wana wa Isaka; Esau, na Israeli.
35 Wana wa Esau; Elifazi, na Reueli, na Yeushi, na Yalamu, na Kora.
36 Wana wa Elifazi; Temani, na Omari, na Sefo, na Gatamu, na Kenazi, na, kwa Timna, Amaleki.
37 Wana wa Reueli; Nahathi, na Zera, na Shama, na Miza.