33 Na wana wa Midiani; Efa, na Eferi, na Hanoki, na Abida, na Eldaa. Hao wote ndio wana wa Ketura.
34 Na Ibrahimu naye akamzaa Isaka. Wana wa Isaka; Esau, na Israeli.
35 Wana wa Esau; Elifazi, na Reueli, na Yeushi, na Yalamu, na Kora.
36 Wana wa Elifazi; Temani, na Omari, na Sefo, na Gatamu, na Kenazi, na, kwa Timna, Amaleki.
37 Wana wa Reueli; Nahathi, na Zera, na Shama, na Miza.
38 Na wana wa Seiri; Lotani, na Shobali, na Sibeoni, na Ana, na Dishoni, na Eseri, na Dishani.
39 Na wana wa Lotani; Hori, na Hemamu; na Timna ni umbu lake Lotani.