4 na Nuhu, na Shemu, na Hamu, na Yafethi.
5 Wana wa Yafethi; Gomeri, na Magogu, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.
6 Na wana wa Gomeri; Ashkenazi, na Rifathi, na Togama.
7 Na wana wa Yavani; Elisha, na Tarshishi, na Kitimu, na Warodani.
8 Wana wa Hamu; Kushi, na Misri, na Putu, na Kanaani.
9 Na wana wa Kushi; Seba, na Havila, na Sabta, na Raama, na Sabteka. Na wana wa Raama; Sheba, na Dedani.
10 Kushi naye akamzaa Nimrodi; yeye akaanza kuwa mtu hodari katika nchi.