24 Wahubirini mataifa habari za utukufu wake,Na watu wote habari za maajabu yake.
25 Kwa kuwa BWANA ni mkuu mwenye kusifiwa sana;Na wa kuhofiwa kuliko miungu yote.
26 Maana miungu yote ya watu si kitu;Lakini BWANA ndiye aliyezifanya mbingu.
27 Heshima na adhama ziko mbele zake;Nguvu na furaha zipo mahali pake.
28 Mpeni BWANA, enyi jamaa za watu,Mpeni BWANA utukufu na nguvu.
29 Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;Leteni sadaka, mje mbele zake;Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu;
30 Tetemekeni mbele zake, nchi yote.Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;