6 nao makuhani Benaya na Yahazieli wenye baragumu daima, mbele ya sanduku la agano la Mungu.
7 Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru BWANA, kwa mkono wa Asafu na nduguze.
8 Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;Wajulisheni watu matendo yake.
9 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi;Zitafakarini ajabu zake zote.
10 Jisifuni kwa jina lake takatifu;Na ufurahi moyo wao wamtafutao BWANA.
11 Mtakeni BWANA na nguvu zake;Utafuteni uso wake siku zote.
12 Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya;Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;