1 Hawa ndio wana wa Israeli; Reubeni, na Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Zabuloni;
2 na Dani, na Yusufu, na Benyamini, na Naftali, na Gadi, na Asheri.
3 Wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela; ambao hao watatu alizaliwa na binti Shua, Mkanaani. Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa BWANA; naye akamwua.
4 Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano.
5 Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli.