11 na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi;
12 na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;
13 na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;
14 na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;
15 na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;
16 na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.
17 Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.