14 na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;
15 na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;
16 na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.
17 Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.
18 Basi Kalebu, mwana wa Hesroni, akazaliwa wana na mkewe Azubu, na Yeriothi, na hawa ndio wanawe wa kiume; Yesheri, na Shobabu, na Ardoni.
19 Akafa Azuba, naye Kalebu akamtwaa Efrathi, aliyemzalia Huri.
20 Naye Huri akamzaa Uri; na Uri akamzaa Besaleli.