37 na Zabadi akamzaa Eflali; na Eflali akamzaa Obedi;
38 na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria;
39 na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa
40 na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;
41 na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.
42 Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.
43 Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.