39 na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa
40 na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;
41 na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.
42 Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.
43 Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.
44 Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai.
45 Na mwana wake Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa babaye Bethsuri.