6 Na wana wa Zera; Zabdi, na Ethani, na Hemani, na Kalkoli, na Darda; hao wote ni watano.
7 Na wana wa Karmi; Akani, yule mwenye kutaabisha Israeli, aliyekosa katika kitu kilichowekwa wakfu.
8 Na wana wa Ethani; Azaria.
9 Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu.
10 Na Ramu akamzaa Aminadabu; na Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa wana wa Yuda;
11 na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi;
12 na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;