7 Na wana wa Karmi; Akani, yule mwenye kutaabisha Israeli, aliyekosa katika kitu kilichowekwa wakfu.
8 Na wana wa Ethani; Azaria.
9 Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu.
10 Na Ramu akamzaa Aminadabu; na Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa wana wa Yuda;
11 na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi;
12 na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;
13 na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;