23 Na wana wa Hebroni; Yeria mkuu wao, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yekameamu wa nne.
24 Wana wa Uzieli, Mika; wa wana wa Mika, Shamiri.
25 Nduguye Mika, Ishia; wa wana wa Ishia, Zekaria.
26 Wana wa Merari; Mali na Mushi; wana wa Yaazia; Beno.
27 Wana wa Merari; wa Yaazia; Beno, na Shohamu, na Zakuri, na Ibri.
28 Wa Mali; Eleazari, asiyekuwa na wana.
29 Wa Kishi; wana wa Kishi; Yerameeli.