10 na Yohana akamzaa Azaria (ndiye huyo aliyefanya kazi ya ukuhani katika nyumba aliyoijenga Sulemani huko Yerusalemu)
11 na Azaria akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;
12 na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Meshulamu;
13 na Meshulamu akamzaa Hilkia; na Hilkia akamzaa Azaria;
14 na Azaria akamzaa Seraya; na Seraya akamzaa Yehosadaki;
15 na Yehosadaki akachukuliwa mateka, hapo BWANA alipowachukua mateka Yuda na Yerusalemu, kwa mkono wa Nebukadreza.
16 Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.