13 na Meshulamu akamzaa Hilkia; na Hilkia akamzaa Azaria;
14 na Azaria akamzaa Seraya; na Seraya akamzaa Yehosadaki;
15 na Yehosadaki akachukuliwa mateka, hapo BWANA alipowachukua mateka Yuda na Yerusalemu, kwa mkono wa Nebukadreza.
16 Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.
17 Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni; Libni, na Shimei.
18 Na wana wa Kohathi walikuwa Amramu, na Ishari, na Hebroni, na Uzieli.
19 Wana wa Merari; Mali, na Mushi. Na hizi ndizo jamaa za Walawi, sawasawa na mbari za baba zao.