32 Na Heberi akamzaa Yafleti, na Shomeri, na Hothamu, na umbu lao, Shua.
33 Na wana wa Yafleti; Pasaki, na Bimhali, na Ashvathi. Hao ndio wana wa Yafleti.
34 Na wana wa Shomeri; Ahi, na Roga, na Yehuba, na Aramu.
35 Na wana wa nduguye Helemu; Sofa, na Imna, na Sheleshi, na Amali.
36 Wana wa Sofa; Sua, na Harneferi, na Shuali, na Beri, na Imra;
37 na Bezeri, na Hodu, na Shama, na Shilsha, na Ithrani, na Beera.
38 Na wana wa Yetheri; Yefune, na Pispa, na Ara.