3 Na Bela alikuwa na wana; Adari, na Gera, na Abihudi;
4 na Abishua, na Naamani, na Ahoa;
5 na Gera, na Shufamu, na Huramu.
6 Na hawa ndio wana wa Ehudi. (Hao ndio wakuu wa mbari za baba zao miongoni mwa wenyeji wa Geba; nao wakawachukua mateka mpaka Manahathi;
7 na Naamani, na Ahoa, na Gera; aliwachukua mateka). Naye akamzaa Uza, na Ahihudi.
8 Na Shaharaimu akazaa watoto katika Bara-Moabu, baada ya kuwafukuza wakeze Hushimu na Baara.
9 Akazaliwa na Hodeshi, mkewe; Yobabu, na Sibia, na Mesha, na Malkamu;