14 Daudi akamwambia, Jinsi gani hukuogopa kuunyosha mkono wako umwangamize masihi wa BWANA?
15 Ndipo Daudi akamwita mmoja wa vijana, akamwambia, Mwendee, ukamwangukie. Basi akampiga hata akafa.
16 Daudi akamwambia, Damu yako na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe; maana umejishuhudia nafsi yako ukisema, Nimemwua masihi wa BWANA.
17 Basi Daudi akamwomboleza Sauli, na Yonathani, mwanawe, maombolezo haya;
18 (kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yashari), akasema,Wana wa Yuda na wafundishwe haya,
19 Walio fahari yako, Ee IsraeliJuu ya mahali pako palipoinuka wameuawa;Jinsi mashujaa walivyoanguka!
20 Msiyahubiri mambo haya katika Gathi,Msiyatangaze katika njia za Ashkeloni;Wasije wakashangilia binti za Wafilisti,Binti za wasiotahiriwa wakasimanga.