10 Aliziinamisha mbingu akashuka;Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.
11 Akapanda juu ya kerubi akaruka;Naam, alionekana juu ya mabawa ya upepo.
12 Akafanya giza hema zake za kumzunguka,Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.
13 Toka mwangaza uliokuwa mbele zakeMakaa ya moto yakawashwa.
14 BWANA alipiga radi toka mbinguni,Naye Aliye juu akaitoa sauti yake.
15 Akapiga mishale, akawatawanya;Umeme, naye akawatapanya.
16 Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari,Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa,Kwa kukemea kwake BWANA,Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.