15 Akapiga mishale, akawatawanya;Umeme, naye akawatapanya.
16 Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari,Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa,Kwa kukemea kwake BWANA,Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.
17 Alipeleka kutoka juu, akanishika;Akanitoa katika maji mengi;
18 Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,Na wale walionichukia;Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu;Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.
20 Akanitoa akanipeleka panapo nafasi;Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
21 BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.