41 Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.
42 Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa;Walimwita BWANA, lakini hakuwajibu.
43 Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi,Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.
44 Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu;Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa;Watu nisiowajua watanitumikia.
45 Wageni watanijia wakinyenyekea;Kwa kusikia tu habari zangu,Mara watanitii.
46 Wageni nao watatepetea,Watatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 BWANA ndiye aliye hai;Na ahimidiwe mwamba wangu;Na atukuzwe Mungu wa mwamba wa wokovu wangu;