43 Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi,Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.
44 Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu;Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa;Watu nisiowajua watanitumikia.
45 Wageni watanijia wakinyenyekea;Kwa kusikia tu habari zangu,Mara watanitii.
46 Wageni nao watatepetea,Watatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 BWANA ndiye aliye hai;Na ahimidiwe mwamba wangu;Na atukuzwe Mungu wa mwamba wa wokovu wangu;
48 Naam, Mungu anipatiaye kisasi,Na kuwatweza watu chini yangu,
49 Na kunileta nje nitoke kwa adui zangu;Naam, waniinua juu yao walioniinukia;Waniponya na mtu wa jeuri.