4 Moyo wake mwenye hekima umo nyumbani mwa matanga, bali moyo wake mpumbavu umo nyumbani mwa furaha.
5 Heri kusikia laumu ya wenye hekima,Kuliko mtu kusikia wimbo wa wapumbavu;
6 Maana kama mlio wa miiba chini ya sufuria,Ndivyo kilivyo kicheko cha mpumbavu.Hayo nayo ni ubatili.
7 Kweli jeuri humpumbaza mwenye hekima,Na rushwa huuharibu ufahamu.
8 Heri mwisho wa neno kuliko mwanzo wake,Na mvumilivu rohoni kuliko mwenye roho ya kiburi.
9 Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako,Maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
10 Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi?Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo.