1 Siku moja, Yesu alikuwa mahali fulani akisali. Alipomaliza kusali, mmoja wa wanafunzi wake akamwambia, “Bwana, tunakuomba utufundishe kusali kama Yohane Mbatizaji alivyowafundisha wanafunzi wake.”
2 Yesu akawaambia, “Mnaposali, semeni:‘Baba!Jina lako litukuzwe;ufalme wako ufike.
3 Utupe daima chakula chetu cha kila siku.
4 Utusamehe dhambi zetu,maana sisi tunawasamehe wote waliotukosea;wala usitutie katika majaribu.’”
5 Kisha akawaambia, “Tuseme mmoja wenu anaye rafiki, akaenda kwake usiku wa manane, akamwambia: ‘Rafiki, tafadhali niazime mikate mitatu,