1 Jumapili, alfajiri na mapema, wale wanawake walikwenda kaburini wakichukua yale manukato waliyotayarisha.
2 Walikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi.
3 Walipoingia ndani, hawakuuona mwili wa Bwana Yesu.
4 Walipokuwa bado wanashangaa juu ya jambo hilo, mara watu wawili waliovaa mavazi yenye kungaa sana, wakasimama karibu nao.