12 Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
13 Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
14 naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
15 na wawe na uwezo wa kuwafukuza pepo.
16 Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
17 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake “Wanangurumo”),
18 Andrea na Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanaani na