46 Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta akifanya hivyo.
47 Kweli nawaambieni, atamweka mtumishi huyo aisimamie mali yake yote.
48 Lakini kama mtumishi mbaya akijisemea moyoni: ‘Bwana wangu amekawia kurudi,’
49 kisha akaanza kuwapiga watumishi wenzake, akaanza kula na kunywa pamoja na walevi,
50 bwana wake atakuja siku asiyoitazamia na saa asiyoijua.
51 Atamwadhibu vibaya na kumweka kundi moja na wanafiki. Huko kutakuwa na kilio na kusaga meno.