24 Watu wa mataifa watatembea katika mwanga wake na wafalme wa dunia watauletea utajiri wao.
25 Milango ya mji huo itakuwa wazi mchana wote; maana hakutakuwa na usiku humo.
26 Fahari na utajiri wa watu wa mataifa utaletwa humo ndani.
27 Lakini hakuna chochote kilicho najisi kitakachoingia humo; wala mtu yeyote atendaye mambo ya kuchukiza au ya uongo hataingia humo. Ni wale tu walioandikwa katika kitabu cha uhai cha Mwanakondoo ndio watakaoingia ndani.