12 Wanafunzi wake wakamwambia, “Bwana, ikiwa amelala, basi atapona.”
13 Wao walidhani kwamba alikuwa amesema juu ya kulala usingizi, kumbe alikuwa amesema juu ya kifo cha Lazaro.
14 Basi, Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa;
15 lakini nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini. Haya, twendeni kwake.”
16 Thoma (aitwaye Pacha) akawaambia wanafunzi wenzake, “Twendeni nasi tukafe pamoja naye!”
17 Yesu alipofika huko alikuta Lazaro amekwisha kaa kaburini kwa siku nne.
18 Kijiji cha Bethania kilikuwa karibu na Yerusalemu, umbali upatao kilomita tatu.