44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo siku ya mwisho.
45 Manabii wameandika: ‘Watu wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
46 Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47 Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uhai wa milele.
48 Mimi ni mkate wa uhai.
49 Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50 Lakini huu ni mkate unaoshuka kutoka mbinguni ili yeyote atakayeula asife.