1 Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke.
2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe.
3 Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake.
4 Mke hana amri juu ya mwili wake, bali mumewe; vivyo hivyo mume hana amri juu ya mwili wake, bali mkewe.