11 Kwa maana, ikiwa ile inayobatilika ilikuwa na utukufu, zaidi sana ile ikaayo ina utukufu.
12 Basi, kwa kuwa mna taraja la namna hii, twatumia ujasiri mwingi;
13 nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika;
14 ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo;
15 ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao.
16 Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.
17 Basi “Bwana” ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.