18 Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina.
19 Nisalimie Priska na Akila, na wale wa nyumbani mwa Onesiforo.
20 Erasto alikaa Korintho. Trofimo nalimwacha huko Mileto, hawezi.
21 Jitahidi kuja kabla ya wakati wa baridi. Eubulo akusalimu, na Pude, na Lino, na Klaudia, na ndugu wote pia.
22 Bwana na awe pamoja na roho yako. Neema na iwe pamoja nanyi.