Flp.
Sura 4:19-23
Swahili Union Version
19Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.
20Sasa atukuzwe Mungu, Baba yetu, milele na milele. Amina.
21Mnisalimie kila mtakatifu katika Kristo Yesu. Ndugu walio pamoja nami wawasalimu.
22Watakatifu wote wawasalimu, hasa wao walio wa nyumbani mwa Kaisari.
23Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu.