1 Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lo lote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.
2 Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.
3 Maana mtu akijiona kuwa ni kitu, naye si kitu, ajidanganya nafsi yake.
4 Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake.
5 Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe.