37 Lakini, ya kuwa wafu hufufuliwa, hata na Musa alionyesha katika sura ya Kijiti, hapo alipomtaja Bwana kuwa ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.
38 Naye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai; kwa kuwa wote huishi kwake.
39 Waandishi wengine wakajibu wakamwambia, Mwalimu, umesema vema;
40 wala hawakuthubutu kumwuliza neno baada ya hayo.
41 Akawaambia, Wasemaje watu kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?
42 Maana, Daudi mwenyewe asema katika chuo cha Zaburi,Bwana alimwambia Bwana wangu,Uketi mkono wangu wa kuume,
43 Hata niwaweke adui zakoKuwa kiti cha kuwekea miguu yako.