13 Na Pilato akawakutanisha wakuu wa makuhani, na wakubwa, na watu,
14 akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;
15 wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.
16 Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [
17 Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]
18 Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.
19 Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina iliyotokea mjini, na kwa uuaji